Ripoti mpya ya Benki Kuu ya Tanzania imethibitisha kuwa sekta ya utalii (travel and tourism), pamoja na kumaliza mwaka wa kalenda wa 2024 ikiongoza katika sekta zote nchini Tanzania kwa kuingiza fedha za kigeni, imeianza tena mwaka 2025 kwa kukua ikisimama kileleni kwa kufikia rekodi mpya ya Dola Bilioni 3.927
Ripoti hiyo mpya ya BOT ya takwimu za Januari 2025 inaonesha mchango wa utalii ni sawa na asilimia 56.8 ya mauzo yote ya nje ya huduma na kiasilimia ni sawa na asilimia 24.1 ya mapato yote ya fedha za kigeni kwa mwaka huo zilizotokana na mauzo ya bidhaa na huduma mbalimbali vikichanganywa kwa pamoja huku kwa mbali ikifuatiwa na madini (Dola Bilioni 3.5) na Uchukuzi (Dola Bilioni 2.4).