Bryan Mbeumo Atua Man United kwa dau la pauni milioni 65

Manchester United imefikia makubaliano na Brentford kumsajili winga wa kimataifa wa Cameroon, Bryan Mbeumo, kwa dau la pauni milioni 65, linaloweza kupanda hadi pauni milioni 70 kutokana na nyongeza ya pauni milioni 5.

Mbeumo, mwenye umri wa miaka 25, anatarajiwa kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu kabla ya kujiunga rasmi na kikosi cha kocha Ruben Amorim, ambacho kinapangwa kuelekea Marekani Jumanne ijayo kwa ziara ya maandalizi ya msimu mpya.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *