Tanzania kuwa na mashirika ya umma yenye ushindani ifikapo 2050

Dar es Salaam. Ifikapo mwaka 2050, Tanzania inajiona kuwa na Mashirika ya umma ya kibiashara yanayoendeshwa kwa uwazi na ushindani, yanayojitegemea na yenye kuleta faida, na yanayovutia uwekezaji huku yakishirikiana kikamilifu na sekta binafsi ili kukuza uchumi.

Dhamira hii imeainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 iliyozinduliwa na Mhe. Rais. Dk. Samia Suluhu Hassan, Alhamis, Julai 17, 2025 jijini Dodoma katika tukio lililohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na sekta binafsi akiwemo Bw. Nehemiah Mchechu, ambaye ni Msajili wa Hazina.

Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) ndio imepewa jukumu la kuhakikisha ndoto hiyo ya kuyajengea mashirika ya umma ya kibiashara nguvu ya kuwa shindani inafikiwa, kwakuwa ndio msimamizi wa uwekezaji wa mashirika hayo.

OMH inasimamia jumla ya Taasisi, Mashirika ya umma na wakala wa serikali 252, ambapo kati ya hizo, 217 zinatoa huduma na 35 zinafanya biashara.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *