wachezaji wa gofu wakulipwa na chipukizi waliofuzu kuendelea raundi ya tatu leo

WACHEZAJI wa gofu 24 wa kulipwa na chipukizi kati ya 68 walioshiriki mashindano ya Lina PG Tour wanatarajia kuendelea na raundi ya tatu ya michuano hiyo inayofanyika viwanja vya klabu ya Gofu Lugalo jijini Dar es Salaam, baada ya kupata alama za juu kuliko wenzao.

Shindano hilo ambalo limeandaliwa na familia ya Said Nkya kwa lengo la kumuenzi Mchezaji wa zamani timu ya Taifa ya wanawake ya gofu, Lina Nkya limeanza Julai 17 na linatarajiwa kumalizika Julai 20,2025.

Wachezaji waliofuzu kuendelea kwa upande wa wakulipwa ni Iddy Mzaki, Juma Said, Athumani Chiundu, Frank Mwinuka, Hassan Kadio, Nuru Mollel, Fadhil Nkya, Abdallah Yusuph, I. Wanyeche, B. Nyenza, Angel Eaton na E. Lembris.

Kwa upande wa wachezaji chipukizi waliofuzu ni Hawa Wanyeshe, Ally Isanzu, Enosh Wanyeche, Gabriel Abel, Salim Shariff, Cloud Mtavangu,N. Mwansasu, M. Nobert, Samwel Kileo, J. Mbunda, Julius Mwinzani, Likuli Juma, P. Emanuel na P. Bonzo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *